Bondia
maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali amefariki dunia
usiku wa kuamkia leo October 31 2016 maeneo ya Kimara DSM, Taarifa
zinadai kuwa alishambuliwa na wananchi baada ya madai ya kuitiwa mwizi.
Taarifa
kutoka kwa Promota Siraji Kaike amesema watu aliokuwa anagombana nao
walimwitia mwizi na wakawa wamemshambulia na baadaye wakawa wamemtupa na
bodaboda waliokuwa wanamjua Thoams Mashali walimuokota na kumpeleka
hospitali ambapo baadaye zilitolewa taarifa kuwa amefariki.










